Uchambuzi wa Wasomi na Maoni yao juu ya Mawaziri walioteuliwa jana na Rais Kikwete....






 “Kikwete amejitahidi sana tena kwa kiasi chake kuwajibika kwa umma, hii inaoneshwa na kuwa tiyari kuwapangua mawaziri na manaibu wao wanaokiuka utaratibu wa ufanyaji kazi kwa Watanzania kwa hili lazima tumpongeze,  amekuwa mstari wa mbele kuwaonesha hao mawaziri wabovu kuwa
utendaji kazi na uwajibikaji vinaenda sambamba, Kuna watu wakishapewa nyadhifa serikalini bwana wanajifanya miungu watu, wanawafanya Watanzania kama ngedere. Wanawageuza kuwa chombo cha kujinyakulia fedha kwa style yoyote ile. Ebu waangalie wale Mawaziri waliokuwa wanahusika na Operesheni tokomeza they were all feeling comfortable and were unwilling to take political responsibility, kwa hili busara za Jakaya zimeonekana” alisema msomi huyo
Lakini what always confuse me ni Uchaguzi na uteuzi wa Mheshimiwa huyu Mkuu wan nchi, hivi kweli anawashirikisha wasaidizi wake vizuri au ndio Business as usual, Haiwezekani mawaziri waeteuliwe mara 2 na wafanye blunder, inabidi tujiliuze kwa nini Kila uteuzi wake unakuwa wa mashaka mashaka, watu wanaoteliuwa unwaona kabisa ni watu wasio kuwa na experience yoyote ya Utawala na utendaji kazi katika taasisi kubwa, Ebu muangalia kama Huyu Philip Mulugo, elimu yake inatatanisha na karirudia kosa lile lile kwa uteuzi wa Juma Nkamia, Juma Nkamia hana uzoefu wowote wa kikazi na utawala, kwanza elimu yake ndogo sana hata hiyo degree hana ndio anaitafuta UDOM kwa sasa, anaenda kuitawala wizara kubwa ambayo ina changamoto nyingi!
Uteuzi wa Dr. Kebwe kuwa naibu waziri wa Afya ni challenge kubwa kwani hata jimboni kwake hajafanya chochote, jimboni harudi Wananchi wa pale wanalia kila kukicha sasa hiyo wizara ya madaktari ataiweza? Ataziweza challenge za akina Ulimboka? Ataziweza Challenge za madaktari wa Muhimbili?
Unazi wake pia umeonekana kwa kumteua mtoa mipasho na Naibu katibu wa chama chake bara Mwigulu Nchemba sijui kama huko Wizarani atapeleka mipasho katika uaandaaji wa  bajeti ya taifa, lazima tuwe tunajiuliza kama Watanzania ni kweli hawa watu wanatufaa au wamepewa nyadhifa kishikaji na kwa kujuana!
Msomi huyo ameendelea kutudokeza mengi kwa masharti ya kutotajwa jina na sisi kama kampuni ya Tanzania Kwanza tutafanya hivo, aliyoyaaongea ni mengi mno mengine yataletwa siku nyingine!