Akizungumza Dar es Salaam jana, Mrema alisema
maudhui ya vitabu hivyo ni kueleza mikakati yake katika kuwatetea
wananchi wa Vunjo kuwakwamua na kero mbalimbali zinazowakabili.
Mrema alisema kitabu cha kwanza kimelenga kuelezea hatima ya wakulima wa kahawa, ambao ndiyo walio wengi Vunjo.
Katika kitabu hicho, Mrema amehoji sababu za Chama
Kikuu cha Ushirika cha Kilimanjaro (KNCU) kuendelea kukopa kahawa za
wakulima, kushindwa kuwalipa mabaki, ushuru na nyongeza za wakulima.
Mrema katika kitabu hicho vilevile amehoji iwapo
kuna ukweli wa KNCU kuidai Serikali fedha za fidia zinazotokana na
mdororo wa uchumi mwaka 2008/09, au kinawahadaa wananchi.
Katika kitabu cha pili, Mrema ameelezea
alichokiita ukweli kuhusu kiwanda kinachojengwa eneo la njia panda ya
Himo jimboni humo, ambacho kumekuwa katika mgogoro baina ya wananchi na
mwekezaji.
Mrema alisema kumekuwa na madai kuwa yeye (Mrema),
anamzuia mwekezaji kujenga kiwanda eneo la Himo ili wananchi wakose
ajira na kwamba ameamua kutumia kitabu hicho kueleza ukweli.
Ndani ya kitabu hicho, zipo barua za malalamiko ya wananchi kwenda kwa Waziri Mkuu na wakipinga ujenzi huo.
na uendeshaji wa kiwanda hicho kinachodaiwa
kimejengwa katika eneo la makazi ya watu huku mwekezaji akikiuka sheria
na kujenga bila kibali.
Vile vile vipo vielelezo toka wizara ya ardhi
vikikubaliana na malalamiko ya wananchi na vinavyomuagiza mkurugenzi wa
halmashauri ya Moshi ahakikishe kiwanda hicho hakijengwi na kama
kimejengwa basi kisimamishwe na mwekezaji alipe faini
Mrema anasema yeye kama mwakilishi wa wananchi hao
atahakikisha anawasemea wananchi wake na kupambana kukabiliana na kero
zinazowakabili wananchi wa jimbo hilo