Lissu : Zitto anaendelea kuwa CHADEMA kwasababu ya Mahakama tu




Akizungumza katika "press conference" ya Chadema na waandishi wa habari iliyofanyika leo Mwanasheria mkuu wa Chadema, Mh.Tundu Lisu alisema kuwa mkakati wa kuwachafua viongozi ni wa siku nyingi ambapo Chama kimefanikiwa kunasa mawasiliano ya Zitto tangu mwaka 2009 alipokuwa akiwasiliana akina Denis Msack wa Mwananchi. Lissu alisema njama hizi ndio zilizopelekea mpaka mashtaka ya Ugaidi ambapo katika mahojiano yake ya Star Tv akiwa na akina Mwigulu Nchemba zitto hakukanusha, pia aliandika kwenye mitandao kuwa Chadema imtose Wilfred Lwakatare
Lissu aliongeza kuwa Zitto mpaka sasa ana magari mawili ya Nimrod Mkono na Mkono mwenyewe ndie amewaambia taarifa hizo. Mkono amewaambia kuwa amempa Zitto hela nyingi sana na Zitto alishiriki moja kwa moja kumzuia mgombea wa Chadema katika Jimbo la Nimrod Mkono wakati Nimrod Mkono alikuwa ni namba sita katika orodha ya Mafisadi iliyotajwa pale Mwembeyanga. 

Lissu alisisitiza kuwa washirika wa usaliti huu na uhaini huu hawakupenda kutangazwa kuwa wao ni Wasaliti na wahaini lakini yeye anasema wale ni Wahaini na Wasaliti. Lissu aliasema kuwa Zitto anaendelea kuwa Mwanachama na Mbunge wa CHADEMA kwasababu ya Mahakama tu na sio kwasababu ya mapenzi ya CHADEMA. 


Mapema Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Slaa akitoa maadhimio ya kamati kuu alisema kuwa Kamati Kuu imeamua kuwavua Uanachama ndugu Samsoni Mwigamba na Dr. Kitila Mkumbo kuanzia tarehe ya jana baada ya maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu. 

Maamuzi hayo ni baada ya kunasa mawasiliano mbalimbali ya Zitto Kabwe na washirika wake akiwemo anayejulikana kwa jina la Chadema Mpya. Dr. Slaa anasema malengo ya waraka wa mabadiliko hayakuwa ya kisiasa tu bali yalikuwa na lengo la kuimaliza chadema na kuwabomoa Viongozi wa Chama. 

Dr. Slaa alisema Kamati Kuu imechukua maamuzi haya kwa uchungu kwasababu CHADEMA haina lengo la kupunguza wanachama bali kuongeza Wanachama hata wanaCCM katika kuharikisha ukombozi wa Taifa letu.

Mwisho

Chama kinawatangazia Wanachama wote na wapenzi wote kutokushiriki mikutano ama shughuli zozote za kisiasa zitakazoandaliwa na Zitto Kabwe na Washirika wake kwa jina la Chama