
TAMBWE.
Simba na Yanga zinakutana katika mchezo huo, huku
ikiwa ikiwa imepita miezi miezi miwili tu tangu iliposhuhudiwa sare ya
mabao 3-3 ya timu hizo katika pambano la Ligi Kuu lililopigwa Oktoba 20
kwenye uwanja huohuo.
Hata hivyo, tofauti na mchezo baina ya timu hizo
uliotangulia, mikwaju ya penalti itatumia kuamua mshindi endapo dakika
90 zitakamilika kwa sare.
Vikosi
Timu hizi zitaingia uwanjani zikiwa na baadhi ya
sura mpya za wachezaji waliosajiliwa wakati wa dirisha dogo la usajili,
ambapo Yanga imewanasa nyota wawili wa zamani wa Simba, kipa Juma
Kaseja na mshambuliaji Emmanuel Okwi, pamoja na kiungo wa Ruvu Shooting,
Hassani Dilunga.
Nayo, Simba imeboresha kikosi chake kwa kuwasajili
makipa wa zamani wa Yanga, Ivo Mapunda na Yaw Berko, kiungo Awadh Juma
aliyemaliza mkataba Mtibwa Sugar na mshambuliaji wa Ally Badru kutoka
Suez Canal ya Misri.Isitoshe, Simba itakayocheza dhidi ya Yanga leo
itakuwa chini ya benchi jipya la ufundi litakalokuwa na kocha mkuu
Zdravko Lugarusic na msaidizi wake Suleiman Matola ambayo walichukua na
nafasi za Abdallah Kibadeni na Jamhuri Kihwelo waliofungashiwa virago.
Uhalisia wa mambo
Yanga iliyokuwa imepiga kambi kwenye Hoteli ya
Protea jijini Dar es Salaam itaingia uwanjani ikiwa inajiamini zaidi
kutokana na kuwa na kikosi chenye wachezaji muhimu wanaozitumikia nchi
tofauti za ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Kwa upande wa Simba ambayo ilijichimbia kambini
Visiwani Zanzibar, ni wazi itajitupa uwanjani, lakini ikiwa na unyonge
unaotokana na mgogoro wa kiuongozi unaoendelea kati ya mwenyekiti wa
klabu hiyo, Ismail Rage na kamati yake ya utendaji.
Kocha wa Yanga, Mdachi Ernest Brandts
akiuzungumzia mchezo huo alisema kikosi chake kipo tayari kukabiliana na
Simba na kuvuna matokeo ya ushindi.
“Tumefanya maandalizi ya kutosha kwa ajili ya
mchezo wa Jumamosi (leo), sina wasiwasi na ubora wa kikosi changu nina
matumaini ya kuibuka na ushindi,” alisema Brandts.
Naye Lugarusic ambaye huo utakuwa mchezo wake wa
kwanza dhidi ya Yanga alisema kikosi chake kimeiva na kitawashangaza
wapinzani wake.
“Najua Yanga wanajiamini sana, lakini mimi nasema wanakosea, itakuwa ni mechi nzuri na yenye ushindani,” alisema Lugarusic raia wa Mcrotia.
“Najua Yanga wanajiamini sana, lakini mimi nasema wanakosea, itakuwa ni mechi nzuri na yenye ushindani,” alisema Lugarusic raia wa Mcrotia.