DR. KITILA MKUMBO AKASIRISHWA NA SHUTUMA ZA KUUTAKA UKATIBU MKUU CHADEMA

Kuna mtindo umeibuka wa watu kuwasemea wenzao mitandaoni bila ridhaa yao. Mimi ni moja ya waathirika wa kusemewa mambo. Sasa kuna mwana JF kaanzisha kampeni ya kutaka mimi Kitila Mkumbo niwe Katibu Mkuu wa Chadema. Ujumbe wangu ni kwamba: Vijana acheni kufanya hizi siasa za bei rahisi. Utaratibu wa kumpata Katibu Mkuu ...wa CDM unajulikana na hii ya kupigiana kampeni kwenye mitandao sio mojawapo. Mnaleta mijadala ambayo haipaswi kuwepo na kusababisha mitafaruku isiyo na maana na kupoteza muda wa kuidhoofisha CCM. Nina kazi kubwa ya kuelimisha vijana wetu katika vyuo vikuu na ninaifurahia kazi hii. Mchango mdogo ninaotoa kwa CDM kwa nafasi niliyo nayo sasa unatosha na ninaridhika.