Mwisho wa uongo ni aibu. Siasa za uongo hazilipi.
Lazima mtu mmoja ajitoe muhanga kukomesha siasa za uongo na utungaji
hekaya. Nimeamua kuchukua wajibu huo kuokoa nchi kutoka kwenye makucha
ya siasa za uongo, uzushi na uzandiki. Iwe fundisho kwa vifaranga na
mama zao. Mabadiliko ni hoja na kusimamia hoja za umma na sio utungaji
wa hekaya dhidi ya washindani wako kisiasa.